Ukweli wenyewe

Nimeangalia kipindi cha kuhusu watoto wa mtaani huko kwenye nchi ya Ghana na kimeniuzunisha sana.
Naamini kwenye ubunufu ndiyo nia pekee ya mafanikio .
Kunaubunufu wa aina nyingi sana hapa Duniani ila kuna watu wengine wameamuwa kutumia Ubunifu kwa njia isiyo ya halali.
Mwanadamu ameamuwa kutengeneza umaskini kama kinga pekee ya kumpatia nguvu.
Kuna watu wengi sana wanaangamia hapa duniani wakati kunawengine wakitumia nguvu ya hela waliyonayo kwa ajili ya kugandamia na kuhakikisha kwamba hawa wengine hawawezi kujipatia hata mlo wa siku.
Bara la Afrika ni Bara la Amani .
Nasema hivyo kwani ndiyo bara pekee lililo kubaliana na tamaduni ya  kila jamii iwe ya Marekani ,Ulaya au Asia .
Imefikia mpaka watu wa bara nyingine haswa Ulaya ,wameamuwa kutumia mfumo huo wa kuwapatia waafrika tamaduni mbalimbali ili waweze kuwagombanisha.
Tunaona sasa waafika wakigombana kati ya Wakristo na Waislam.Ukiangalia kiundani Ukristo na Uislam si Tamaduni ya Mwafrika.Hizi ni tamaduni tulizoletewa na sasa zinatufanya tunabaguwana .
Naamini wanadamu tunapaswa tuamini kwa Mungu mmoja na njia pekee ya kuwa karibu ni Upendo.
Ila wanadamu hatupaswi kulazimishana tuabudu kwa wakti mmoja au katika nyumba moja.Hii mbinu iliyoletwa na wakoloni kwa ajili ya kututawala.
Kama msanii ninaamini Afrka inawabunifu wazuri tu ,naamini waafrika tunaweza na wakati umefika wa sisi wenyewe kuendeleza bara letu.
Waafrika wote tunatakiwa tuwe kitu kimoja.
Aksante

Kommentarer

Populära inlägg