mmbando kennedy Painting

Mazingira tunayoishi ni kichocheo cha maisha yetu.Nimekuwa nikiangalia na kufuatilia jinsi mazingira yanavyopata misukosuko mbalimbali huku bianaadam wakijidanganya kwa mipango mbalimbali huku wakijikweza kuwa wao ni watunzi wa mazingira huku ni waongo tu kama vile vibaka walivyo waongo.
Inapofikia sehemu mtu haoni tena umuhimu wa mazingira yanayomzunguka kwa kisingizio ni mipango mbalimbali isiyotekelezeka.
Kumekuwa na wimbi kubwa la kuangamiza wanyama waliopo nchi za Afrika mashariki huku wahusika wakiwa wanajivinjari huru mbele ya mkono wa sheria.
Najuwa kwamba ni kitu cha ajabu kufikiri ila mimi naamini kwamba kuna binaadam na kuna wasio binaadam.
Kwa nini ninaamini hivi?
Kuna mengi sna ya kuchunguza ili ujuwe ukweli wa maisha yalivyo na utajuwa vikundi vya jamii kwa kuangalia ishara zao.Kuna kundi la jamii linalo kiuka ubinaadam na kwa kiasi kikubwa linakuwa ni kundi lenye nguvu.Kwa sisi tunaoamini Mwenyezi Mungu tunaamini hili ni kundi la mashetani kwenye miili ya uanadamu.
Kundi hili lipo kwenye aina zote za makundi bila ya kujali rangi zao wala nchi wanayotokea.Kundi hili hutambuana kwa ishara .
Ishara ?
Ishara inaweza kuwa ni lugha au michoro ambayo wao huelewa .Mfano anaweza kuja mtu kuwekeza Tanzania na pindi anapokuwa Tanzania atakuwa anatafuta mtu wa ishara zake .Mtu huyu atajaribu kwenda kwenye akundi ambayo anaweza kukutana na mtu wa aina hii
Pindi wanapokutana wanakuwa ni watu wenye ujuzi tofauti ila wanatokea kwenye asili moja

Kommentarer

Populära inlägg