KWENYE ONYESHO LA UTALII LEO

Kumekuwa na onyesho la utalii lililopewa jina la Travel Taste hapa Orebro nchini Sweden.
Onyesho hili limewakutanisha wadau mbalimbali kutoka nchi mbalimbali ambao ni kutoka makampuni ya utalii na wapenzi wa Safari.
Kampuni ya Kennedy ambaye ni Msanii wa kimataifa wa sanaa za ufundi kutoka Tanzania imepata nafasi ya kuonyesha sanaa katika maonyesho haya pamoja na kuzungumzia vivutio vilivyopo nchini Tanzania.
Katika Onyesho la leo kumekuwa na mwamko mpya wa kuweza kushiriki kwa baahi ya makampuni kwenye kuleta watalii wengi nchini Tanzania ili kusaidia kwenye kukuza kipato cha Wananchi.
Pia wadau wengi wameonyesha kuvutiwa na kuwa na hamu ya kuona msanii alipotokea na kuweza kusafiri nae kwenda kuandalia mandhari ya nchi pamoja na vitu vingine kama vile utamaduni n.k




Kommentarer

Populära inlägg