Matukio Ghafla.


kwenye meli
mazungumzo na vijana
chakula kizuri
kuhusu kuwa na pasipoti kwenye safari ndani ya
Rap kwa ufupi
Ilikuwa ndani ya meli tukiwa tunasafiri kwa ajili ya mapumziko mafupi.Kulikuwa na watu wengi na wengiwao ni watoto na wazazi.
Vijana wengi walionyesha kuwa na mtazamo tofauti na ule wa wasichana ingawa wasichana walikuwa wanalewa na kujaribu kujificha na kulewa zaidi.Vijana walikuwa wanatumia vitambulisho vya kaka zao kwa ajili ya kununulia pombe na kisha kujificha na kunywa na wasichana.
Niliamuwa kuzungumza na kijana wa kwanza.Kijana alisema kuwa yeye anasafiri na mama yake na alianza kulaumu matokeo ya vita ya wenyewe kwa wenyewe kule nchini kwao Mashariki ya kati.
Alianza kwa kusema , kaka angalia jinsi walivyokuwa wajinga wanauwa vijana wadogo hata kabla hawaja fumbuwa macho yao.Hii ni jinsi alivyokuwa anaizungumzia nchi ya Sirya.
Aliendelea kulaumu jinsi nchi za magharibi zinavyojihusisha kwenye migogoro yao na kwa madai ya kwamba wapo kwenye biashara ya mafuta.
“wanaanzisha migogoro Sirya kwa ajili ya kupata njia ya kuchukuwa mafuta ya Iraki” aliendelea kusema.
Tulikuwa tunaongea na ghafla tukaletewa chakula.Chakula kilikuwa kizuri sana na kijana aliendelea kwa kusema anampenda mfalme wa Sweden kwa sababu anajali watu wake.
Angalia myronna ni sehemu ya kuweka nguo zilizochakaa kidogo na kisha kuwasaidia watu wasio na uwezo.Aliniuliza kama na sisi tunafanya hivyo kule Tanzania na nilimjibu hapana.
Kwa haraka niligunduwa na sisi tulipaswa kufanya hivyo kwani tuna watu wenye uwezo wa kubadilisha nguo kila mwezi na si wangeweza kuzi gawa nguo za zamani kwa watu wasio na uwezo? Nilienedelea kujiuliza.
Ghafla tulielekea kwenye sehemu ya juu ambapo kulikuwa na vijana wengi wakicheza mziki,wengi wao walicheza na wazazi wao.Kijana niliyekuwa nae alianza kucheza na ghafla alianza kucheza na watoto wa kike walio sawa na umri wake.Ghafla mzazi mmoja laimuuliza kwa nini anacheza na wale watoto wenzie na kama anaweza kujuwa kuwa wao ni watoto.Yule kijana akamjibu alikuwa anacheza na wale watoto kwani na yeye alikuwa mtoto pia.Nilimuuliza alikuwa na miaka mingapi na alijibu mikaka kumi na sita.Na kweli wale vijana wengine walikuwa na mika kati ya kumi na sita mpaka saba.
Aliendelea kusema kuwa yule aliyemuuliza akupenda kumuona anafuraha kwani alikuwa nanonekana kwa sura ya kiarabu.
Nilimshauri kutulia na ni vizuri akaenda kukaa na wazazi wake mpaka hasira zitapopunguwa.Najuwa kuwa inauma kuona upo kwenye nchi yako na unapangwa kwenye makundi kutokana na muonekano ulio nao.
Kijana alienda kuonana na wazazi wake na hakurudi mpaka tulipokutana kesho yake.

Ghafla walikuja rafiki zake .”hi brother “ walisema na mimi nikawajibu “hi” waliendelea kuniuliza kama ningewaimbia baadhi ya nyimbo mfano Bob Malrey ,Eminemy ,J Z,0 Cent na nyingine nyingi.
Niliwajibu ninaweza kama nina maneno yao ila ninapendelea kuimba nyimbo zangu mwenyewe.
Waliniomba niwaimbie na nilianza kwa kurap nyimbo kadhaa.
Waliniuliza kama nyimbo zipo kwenye Tv.

Leo ni siku ya ijumaa na nimeendaz Upsala kwa ajili ya kesi ya madai ya ugomvi kati yangu na watu kadhaa.Nimeamuwa kusoma baadhi ya vitabu vya sheria ili kuona ni jinsi gani ya kuelezea tukio.
Kumekuwa na matatizo ya kubakikiwa kesi kwa watu wenye asili ya ugeni,nimeamuwa kusoma sheria zao ili nielewe na kuamuwa kujilinda na kulinda jamii ya waafrika wanaiokuja.washichana wengi wametumia sheria ya unyanyaswaji kwa ajili ya kujiingizia kipato haswa kwa watu wageni wasiojuwa sheria zao.Tumekuwa tukinyanyaswa kwa namna moja au nyingine juu ya kuwa sisi ndiyo wenye kosa hata kama si sisi tumetenda kosa.
Wadada wawili wanatoka kwenye basi ,wanaanza kurumbana na bibi mmoja aliyekuwa anazungumza na mimi.
Nilipowauliza ni kwa nini wanamtukana yule bibi walianza kunitishia uhai kwa kusema watanivamia .
Ghafla ulianza ugomvi na mimi nilipigwa chupa mkononi na mkoni uliumia.Watu waliokuwa pale walionyesha kunichukia na ghafla walikuja polisi na kunikamata.
Niliwauliza ni kwa nini na walishindwa kueleza sababu.Walikuwa wanasema nimelewa wakati sikuwa nimelewa.
Niliwekwa kituoni mpaka asubuhi,ilipofika asubuhi niliojiwa na dada mmoja mwenye nguo za Polisi ,aliniangalia mkono na aliona umeteguka.
Niliamuwa kwenda Hospitali na nikafanyiwa uchunguzi kwa njia ya e ray.Daktari aliamuwa wanifanyie opasuaji.
Nilifikiri inaweza kuwa njia ya kuharibu mkono wangu kwani ndiyo ninaofanyia kazi.Niliamuwa kwenda Stockholm .Niliwasiliana na watu ninaofanya nao kazi .Walinisaidia kunipeleka kwenye ospitali ya mjini Stockholm.
Nilionana na daktari mwingine na alinifanyia uchunguzi kisha akasema atajaribu kuninyoosha mkono
na nisingehitaji upasuaji.
Nilifanyiwa unyyoshaji na kisha nilienda nyumbani .Nilirudi kwa daktari baada ya wiki mbili na aliniangalia tena na kuninyoosha mkono na nilirudi tena baada ya wiki mbili na kutolewa ogo.
Nilipewa msharti ya kufanya Mazoezi na baada ya mda nilipona.

Kwenye ndoto kuna mambo mengi ya msingi na nimeamuwa kufuatilia na kulinganisha ndoto na hali alisi ya kawaida ya mwanadamu.Matukio mengi ya kwenye ndoto yanalinga na ya hali halisi ya mwanadamu wa kawaida.
Kuna watu wamesema tupuuzie ndoto hali kwamba ndoto inakubalika hata mahakamani.Kuna watu wameota matendo na kuthibitisha katika hali ya kawaida.
Najaribu kelezea ndoto kwenye michoro yangu na nimekuwa nikiweka alama zote zinazotokea kwenye ndoto.Najuwa kwamba ninakazi kubwa ya kuchora yote yaliyo tokea kwenye ndoto kwani ni mengi na yote ni ya maana.
Moto mkubwa unatokea kwenye mkono na ghafla najitaidi kuangalia na ninaona ni moto mkali na unanagaa zaidi ya almasi.Sauti inasikika ikisema tumia nguvu uliyonayo ,unanguvu ya kufanya maajabu .Najiuliza kama nimeshatumia nguvu na najuwa kuwa nimekuwa nikidharau na kupuuza nguvu iliyo ndani yangu.
Nimekuwa nikijenga furaha kwa watu wasiona umuhimu kwangu na kuwaacha wale walio na umuhimu.
Watu wa Mungu ni wengi na wenye furaha ,tumekuwa tukijihusisha kwenye matendo ya kuridhisha watu wasio na mapenzi ya kweli.Tumepoteza mda mwingi kuwaridhisha watu wasiotosheka na fadhila.
Taifa la Mungu linatuhitaji ,kweli ya kweli idumu kwa walio na kweli ,maji chumvi na maji sukari hayashikamani
Naamka na nasikia sauti ikisema ,nasikiliza na kuthibitisha ni sauti ya kweli na inasisitiza juu ya kutumia nguvu kubwa ya maajabu.Najiuliza na naona mwanga mkuu kwenye mwili unaangaza na unapotelea ndani ya mwili.
Nguvu kuu ni ya maajabu , nguvu kuu ya kuhamisha milima na miji mikubwa na kupeleka kwenye sehemu za mapambano.
Nguvu kuu ya kutikisa miji mikuu na kuangaza sehemu zenye giza.Nguvu kuu ya kutikisa walio na uwezo wa kishetani na kuwaelekeza kwenye Upendo wa mwenyezi Mungu.Nguvu kuu ya kulinda na kuhifadhi vile vyote vyenye kuheshimu na kulinda haki ya mwanadamu.

Haiitaji kumgusa mtu na kufanya miujiza kwani miujiza haina mipaka.Tunafanya miujiza duniani na hata kwenye mbingu.
Ni vigumu kuamini kwenye jambo lenye ukweli .Kwenye mwanga kuna mwanga na mstari kwenye mwanga na ncha ya mwanga kuwa mwanga na giza kupambana na mwanga.
Kitabu chao cha wenye kudhani wanauwezo kinageuka juu chini nikiweka kitandanai kwangu,ishara ya juu chini ni ishara ya kuonyesha nisiamini mambo wanayonifunza na nianze kufuata na kufanya mambo yangu.
Wao wana jaribu kutafuta nguvu uliyo nayo ili watumie kwa ajili ya jamii yao na wewe unanguvu kwa ajili ya kukomboa jamii yako.
Kuna uwezo wa kuchasaidia wenzetu ila si kwa njia ya kutudanganya na kuchukuwa kila tulicha nacho kwa faida yao binafsi.


Nilikuwa na rafiki zangu tukiimba na nilikuwa naimba kwenye jukwaa lenye watu wengi wa kila aina.
Natumia nguvu ya miujiza na rafiki yangu mmoja aligunduwa na tuliimba kwa pamoja.Wengine watatu walijaribu lakini walishindwa .Tuliimba na kuendesha baiskeli jukwaani .Niliwasikia wakinongona na kujiuliza tulipata wapi nguvu.Watu wengi walishangilia na tulipata wafuasi wengi.
Niliona watu wa zamania niliosoma nao upande wa pili ,baadhi ninawakumbuka na baadhi siwakumbuki.Kuna waliofurahishwa na waliojiuliza ,wengine walijaribu kufananisha ila walishindwa.
Kundi kubwa la watu lilitufuata na tulipanda gari na kuelekea makwetu.Nilimfundisha rafiki yangu lugha ngeni na tulitumia kwenye nyimbo ,watangazaji wengi walifurahishwa na tunzi zile walijaribu kuwasiliana nasi .

Sfarini kwenda Finlandi na boti ya Silja.
Tulifika kwenye mapokezi ya biti mapema na mimi na mwanangu Isaki tulikaa kusubiri turuhusiwe kuingia ndani.
Joyce na Rikard walikuja na watoto zao Arvin na Arvid pamoja na dada yake Joyce.
Tulianzan safari saa kumi na mbili jioni.watu wote waliingia kwenye Boti na walionekana kuwa na furaha wakubwa kwa wadogo.
Tulienda kununuwa vitu vya kula kwenye duka na baadae Tulienda nje kwenye maonyesho mbalimbali.
Kulikuwa na bendi ya mziki mwanana kutoka Brazil na watu wengi waliangalia michezo yao ya kapoera pamoja na mwimbaji wao mashuhuri wa kike.
Tulizunguka boti nzima niliona vijana mbali mbali wakiwa wamechoka kutokana na kunywa pombe sana.
Tuliwapeleka watoto kwenye bwawa la kuogelea na walifurahi sana.
Hamna kitu cha umuhimu kwa watoto kama kucheza na mumi na kucheza kwenye sehemu za kuchezea watoto na kisha kwenda kuogelea.
Nakumbuka sisi watoto wa kiafrika hatukuwa na sehemu kama hizi kwa kipindi tulichokuwa tunakuwa kwenye miaka ya themanini.
Nakumbuka siku moja ilitugharimu tutafute sehemu ya kychezea na tulizunguka eneo kubwa na tuliishia kuokota silaha badala ya kupata sehemu ya kuchezea.
Wtoto wanahitaji kupata sehemu za kuchezea ili kuweza kutumia mda wao wa utoto kucheza na kuongeza ujuzi.

Afarai ya basi Swedbuss
Ilikuwa siku ya jumapili baada ya kumrudisha mwanagu nyumbani.Tuliamuwa kurudi nyumbani jumapili baada ya safari nzuri ya boti.
Nilipata usafiri wa Swed bus ni safari nzuri kwa kuwa wanamabsi mazuri .Nimekutana na watu wengi wenye kuoneka kama wametoka kwenye sherehe mbali mbali siku ya jumapili na sasa wanaamuwa kurudi manyumbani kwao.
Kunauwezekana mkubwa wa kusafiri na mabasi kwa hali nzuri ya kuonekana mtalii ikiwa tu mabasi yanuwezo mzuri na yamejengwa kwenye ubora unaotakiwa.
Usafiri wa mabasi hapa ni mzuri sana kwa sababu mabasi yanaubora wa kiwango cha juu ukilinganisha na Tanzania ambapo kuna matatizo makubwa kwenye huduma ya usafiri.
Wawekezaji wa nchi maskini hawajali ubora wa huduma wanazotowa kwa kuwa wamekuwa wakitumia vifaa vichakavu na wamekuwa wakihatarisha maisha ya wasafiri wengi ikiwa ni pamoja na watalii kutoka nchi mbali mbali.
Tunapishana na magari mbali mbali yenye kuonekana tufauti tofauti.Magari mengi ni ya familia na yanaonekana kuaharakisha kutokana na watu kwenda makazini kesho.
Watu wengi wanatumia siku za mwisho wa wiki kutembelea familia zao huku wengine wakitumia magari binafsi.
Usafir wa magari binafsi ni mzuri pia kwa watu wasiotumia vilevi.Ni usafiri wa kuharakisha harakisha kwa wale wanaotumia vilevi.
Napenda kutumia mabasi kwa sababu hayaharakishi yanapokuwa njiani na yanafuata ubora na matakwa ya Abiria.
Tunapita kwenye misitu karibia na Arboga na tuanaona nje kunakuwa na giza nene kutokana na wingi wa misitu.
Misitu ya nchi za skandinavia ni ile ya kupandwa na inaonekana kufanana.Ni misitu yenye matawi madogo ila imebanana kwa hiyo ni vigumu kupitisha mwanga.
Najuwa kuwa kuna giza jingi wakati wa kipindi cha baridi na mwanga mwingi wakati wa kipindi cha kiangazi.

Kumekuwa na vifaa vingi vya kuakisi mwanga barabarani kipindi cha baridi ili waendesha magari yaweze kuona kule yanapoelekea.
Ok , niwakati wakutambuwa na kuelewa tunaishi na viumbe wa aina mbali mbali .Moja wapo ya njia ya kuwatambuwa ni kujuwa jinsi wanavyofikiri na kurekodi matukio wanayofanya.Nimekuwa nikitakia mema jamii yangu na ninaelewa inawezekana kujaribu kufanya jambo la umuhimu kwa pamoja kama mambo haya ninayoyaona hapa.
Miundo mbinu ni moja ya mtego uliokuwepo kwenye karne hii ya 21 .Watu wengi wanaingia kwenye matatizo ya kuchanganya matukio mbilimbali huku wakidhani ni mabadiliko ya kisayansi
Kuna vijana wengi wanakumbwa na tabia ya kufanya mambo yasiyo na mwongozo huku nchi nyingi haswa za bara la Afrika zinamigogooro ya kijamii pamoja na mabadiliko ya kisayansi.

Kumekuwa na trik wanayoifanya waandaaji wa huu utumwa mamboleo haswa kwa jinsi walivyobadilisha mazingira ya kimasaa pamoja na jinsi watu watakavyofanya kazi zaidi ya mda maalumu walioupanga.
Watu wengi wamejichanganya na uovu wa shetani kwenye nyumba za kawaida mpaka nyumba za ibada.
Najuwa inakuwa vigumu kuelezea jinsi mtu anaweza kujuwa anachohitaji kufanya na jinsi ninavyoona wao wanavyopanga ingawa kunauwezekano wa kugunduwa kwa uwezo wa roho mtakatifu.
Fikiria jinsi mazingira yanavyoharibiwa na wale waliovaa ngozi ya ubinadaam.Wasiyojuwa hili wanakaa chini yao na kuharibu ndugu zao kwa msingi wa kutetea kile wanachojuwa wao.

Kumekuwa na miradi ya kuuwa kile kinachotufanya tuwe wanadaamu na kupromoti au kutangaza kile kisicho na uhai na uanaadam.


Najuwa wengi wanachukia kwa kuwa wanaukweli ndani ya mioyo yao.Wanajuwa wanachokifanya na kwa uelewa wa wasiojuwa wanawatumia kuharibu vile vizuri tulivyojaliwa na mwenyezi Mungu.
Mungu ni upendo na upendo wa kweli usio na mwisho wala mwanzo.Ni vigumu kuelezea kwa lugha ya kawaida .Unatakiwa utambuwe kweli iliyo huru na ujuwe heshima yetu kwa muumba wetu ni ufunguo wetu wa kuishi maisha matakatifu.
Kumekuwa na mvutano wa watu wema na wabaya na kumekuwa na mchanganyo wa kufanya mambo matakatifu kwenye mambo yasiyo matakatifu .
Binadamu anaishi na shetani kwenye mazingira ya mkataba wa siku hizi za mwisho.Binadamu amesaliti matakwa ya mwenyezi Mungu na kuingiza matakwa yake na ya shetani kwenye maisha ya kawaida ya binadamu.
Hii ni kosa kwa sababu kwa nini Matakwa ya binaadamu na yashetani yanakubalika kwa urahisi na si matakwa ya Mungu.
Kumekuwa na kutokukubaliana na mambo mema tokea zambi ya kwanza aliyofanya mwanadamu.Mambo mema yanatumiwa kama mabay na mabaya yanatumiwa kama mema.


Kommentarer

Populära inlägg